
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene
Badala yake, ameutaka Uongozi wa Halmashauri zote nchini hususan Halmashauri ya Mpwapwa kuhakikisha inaachana utaratibu huo, iajiri wataalam wa fani ya ujenzi kwa ajili ya kusimamia miradi yote itakayokuwa ikitekelezwa katika Halmashauri hiyo ili iwe ya viwango vya ubora kama ambavyo baadhi ya Halmashauri zingine zinafanya.
"Kwa sasa majengo yetu yanajengwa na walimu na madaktari na badala ya kujengwa na wahandisi wa ujenzi, hili halikubaliki hata kidogo," amesititiza Mhe.Simbachawene
Ameweka angalizo kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa imekuwa haifanyi vizuri katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi kutokana na usimamizi hafifu kwa sababu Wasimamizi wanaopewa jukumu hilo sio taaluma yao.
Amefafanua kuwa walimu au madaktari wanaosimamia miradi hiyo ujenzi sio kwamba ni wabadhirifu lakini kwa kuwa sio taaluma yao hivyo ni vigumu kuona na hata kushauri pale ujenzi unavyojengwa chini ya kiwango.
Amesema limekuwa ni jambo la kawaida kama mradi wa afya unatekelezwa basi msimamizi wa ujenzi atakuwa Daktari, vivyo hivyo kama ujenzi wa madarasa basi msimamizi atakuwa Mwalimu