
Mamelod wamemaliza wakiwa nafasi ya tatu wakiwa wamekusanya alama nne, alama ambazo wamezipata baada ya kushinda mchezo mmoja dhidi ya klabu ya Ulsan HD FC kutoka Korea kusini huku akitoa sare dhidi ya klabu ya Fluminense na kufungwa dhidi ya Borussia Dortmund, hata hivyo hii ndiyo timu kutoka barani Africa iliyokusanya alama nyingi zaidi wakiwa wamekusanya alama nne.
Inafuatiwa na klabu ya Esperance ya Tunisia ambayo imekusanya alama tatu hii ni baada ya kushinda mchezo mmoja dhidi ya klabu ya Los Angeles FC kutoka Marekani huku wakipoteza dhidi ya Chelsea na Flamengo kutoka Brazil.
Klabu ya mwisho ni klabu ya Wydad Casablanca ambayo mpaka sasa imecheza michezo miwili dhidi ya Juventus na Manchester city na kupoteza michezo yote.
Leo Wydad Casablanca wanakamilisha ratiba dhidi ya Al-Ain kutoka United Arab Emirates, Jambo linalosubiriwa kwa hamu ni kuona kama Wydad Casablanca watafanikiwa kukusanya walau alama moja katika michuano hii.