
Zoezi hilo la kusimika Bendera liliongozwa na Brigedia Jenerali Salumu Mnumbe ikiwa na lengo la kusherehekea Maadhimisho ya Miaka 61 ya Uhuru wa Nchi yetu Tanzania na kuhitimishwa na Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu.
Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) katika kusherehekea Uhuru wa nchi yetu limekuwa likiandaa zoezi hili Kila mwaka kwa kushirikiana na wadau, Mashirika ya Kiserikali, na binafsi kupandisha wageni katika kilele hicho cha Mlima Kilimanjaro zoezi ambalo huongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).