Jumatano , 7th Sep , 2022

Imeelezwa kuwa uwepo wa  maendeleo ya  huduma za kidigitali nchini umepelekea ongezeko la mauzo ya bidhaa za maudhui mtandaoni ikiwemo kwa kampuni  ya mawasiliano ya simu za mkononi nchini ya Tigo ambapo katika robo ya mwisho ya mwaka zimetajwa kuongeza wateja zaidi ya milioni moja.

Moja ya kamouni hizo ni kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya tigo ambapo katika kipindi cha robo ya mwisho ya mwaka imeongeza watumiaji kwa zaidi ya asilimia mia moja hali iliyopelekea kuingia mkataba na moja ya kampuni za uuzaji maudhui ya wasanii ya boomplay kama ambavyo  wiliamu mpinga kutoka tigo anavyo eleza.

Kwa upande wake mwakikishi wa boomplay nchini  Natasha  Stambuli  amesema kwa sasa soko la maudhui mtandaoni limekuwa likikua hadi kufikia watumiaji zaidi ya milioni 12 kwa mwezi huku kwa upande wa boom play ikiwa imesha fikik8sha wateja milioni 85 kwa mwezi.
Nao baadhi ya vijana waliojajiri kupitia maudhui ya mtandaoni ikiwemo nyimbo wamesema uwepo wa nafasi hiyo utasaidia kuongeza wigo wa wateja na wafuasi ambao watasaid8a kuongeza kipato