Jumatatu , 18th Apr , 2022

Viongozi Wakuu wa biashara kutoka nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki, wanapanga kufanya ziara ya kibiashara kueleka nchi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo mapema mwezi ujao.

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Biashara ya jumuiya hiyo (EABC), Bw.John Bosco Kalisa.

Lengo la ziara hiyo ni ni kuvumbua nafasi za kibiashara zinazopatikana nchini Congo 

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Biashara ya jumuiya hiyo (EABC), Bw.John Bosco Kalisa,  amesema kuwa mara baada ya Rais wa  Congo  Félix Tshisekedi kutia saini hati ya makubaliano ya kujiunga na jumuiya hiyo, mpango uliopo ni kukuza biashara baina ya nchi hizo 
 
Wanapanga kusafiri wiki ya kwanza ya mwezi May na wanatamani sana kuwaona wafanyabiashara  kutoka  Congo, amesema Kalisa na kuongeza kuwa 
Kila upande upo tayari kwa ziara hiyo, na mpaka sasa tayari tumeshaanzisha mwingiliano mzuri na shirikisho la wafanyabiashara wa Congo, wamekubali  , amesema Bw. Kalisa akielezea pia mbali na kutembelea mji mkuu wa Kinshasa, pia viongozi hao watatembelea majiji ya mashariki mwa nchi  ya Goma na Bukavu.

Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo  Peter Mathuki, amesema kwamba vijana wanaweza kutazama fursa kwa wakati  katika ukanda huu ambao sasa una wanachama 7 wa jumuiya 
 
Nchi ya Congo inaongoza duniani kwa uzalishaji wa madini ya  cobalt, ambayo ni muhimu sana katika uzalishaji wa betri za kuchaji kwa ajili ya magari ya umeme na pia ni malishaji mkuu wa  madini ya  kopa.