Jumapili , 8th Aug , 2021

Msanii wa singeli anayetamba kwa sasa Kinata MC anasema njaa ndio zimemfanya kuimba singeli ya 'do lemi go' kwa kutumia lugha ya kiswahili na kingeereza mwenyewe anaiita singelish.

Msanii wa singeli Kinata MC

"Elimu yangu nimeishia kidato cha nne na muziki ni talent yangu niliyokuwa nayo kabla, njaa inatisha kuimba kiingereza kwenye singeli imetokana na njaa,ile inaitwa 'singelish' unachanganya kiswahili na kiingereza kwenye mtindo wa kuimba singeli"amesema Kinata MC

Ngoma yake ya 'do lemi go' aliyomshirikisha Ibraah kutoka Konde Gang bado inafanya vizuri kwenye vituo vya radio na tv, pia ina views Milioni 1.5 mjini Youtube.