Jumatatu , 11th Mei , 2020

Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba, amesema sababu ya kuadimika kwa Sukari nchini, imechangiwa na uwepo wa Corona, baada ya Tani elfu 40 za Sukari zilizoagizwa kutoka nje ya nchi, kukwama katika nchi husika baada ya nchi hizo kufunga mipaka yake.

Sukari

Naibu Waziri Mgumba ametoa kauli hiyo wakati akigawa Tani moja kwa waumini wa dini ya Kiislam, ambao kwa sasa wako kwenye mfungo waMwezi Mtukufu wa Ramadhan, zoezi ambalo limefanyika katika Shule ya Sekondari Mbuyuni iliyopo Morogoro.

"Sukari ambayo imeagizwa iko Bandarini kwenye nchi husika, wakati inataka kuja ndiyo janga hili la Corona likaja, badala ya mzigo wote kuja nchini kwa mara moja ikabidi waagize kidogodogo" amesema Naibu Waziri Mgumba.

"Nichukue nafasi hii kutoa onyo kali kwa wafanyabiashara ambao wanauza sukari kwa bei kubwa" ameongeza Waziri Mgumba.