
Dezire
Desire amesema kuwa, anamtambua Michael na hafamu chochote kuhusiana na mwanaume anayefahamika kwa jina Juma Seiko ambaye hivi karibuni aliibuka na kujitambulisha pia kama baba wa mtoto wa mwanamuziki huyu na kuzua mkanganyiko mkubwa.
Katika maelezo yake, Desire ambaye anajikwamua kusafisha jina lake, amemshangaa Juma Seiko, na kuhoji ni wapi mwanaume huyu alikuwepo wakati wote mpaka sasa alipoamua kuibuka kujitangaza kama baba wa mtoto wake.