Jumapili , 27th Nov , 2016

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni, amesema askari wanaojihusisha na vitendo vya rushwa na kushindwa kusimamia sheria wajiondoe kabla ya kuondolewa kwa fedheha.

Masauni aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Paza Sauti kwamba serikali haina mchezo kwa kuwa itawachukulia hatua watendaji ambao watashindwa kusimamia sheria.

“Wale ambao wanajijua ni wapokeaji wa rushwa ni bora wakaacha mara moja kabla ya kuwekwa pembeni maana hatutawafumbia macho,” alisema Masauni.

 

________________
Kumpigia KURA msanii unayempenda kwenye #EATVAwards Bofya hapa https://www.eatv.tv/awards