Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zuberi Katwila ajiuzulu ukocha Mtibwa Sugar

Jumapili , 18th Oct , 2020

Uongozi wa Mtibwa Sugar umethibitisha kuwa kocha Zuberi Katwila, amejiuzulu nafasi yake kuanzia leo Oktoba 18, 2020 baada ya kuwasilisha barua.

Zuberi Katwila

Akizungumza na East Africa Radio, Afisa Sheria na Utawala, Sabri Aboubakar amesema uamuzi wa Zuberi kuondoka klabuni hapo ni wake binafsi na wao kama uongozi wamebariki baada ya pande zote mbili kuridhia.

Sababu za kujiuzulu kwa kocha huyo hazijawekwa wazi kufuatia makubaliano ya pande hizo mbili kukubaliana kuwa ni siri.

Katwila amejiuzulu ikiwa ni siku chache baada ya Mtibwa kupoteza mchezo wa tatu mfululizo wa ligi kuu na mara ya mwisho walinyukwa 2-0 na Gwambina.

Katwila amedumu katika klabu ya Mtibwa tangu mwaka 1999 akiwa mchezaji kabla ya kugeukia ukocha kwa miaka 8, huku mitatu katika hiyo alikua kocha mkuu wa wakatamiwa hao.

Mikoba yake kwa sasa imeachwa kwa Vicent Barnabas ambaye alikua msaidizi wake tangu kuanza kwa msimu.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava