Kelvin Yondani
Beki na nahodha wa zamani wa Yanga Kelvin Yondani ataikosa mechi ya Yanga dhidi ya Mtibwa Sugar itayopigwa Jumatano hii katika uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro kutokana na kuwa na matatizo ya kifamilia.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa kitengo cha Habari na Mawasiliano, Hassani Bumbuli na kusema kuwa ni kweli nyota huyo hatokuwa miongoni mwa kikosi ambacho kinaondoka leo majira ya saa saba mchana huku akiweka wazi kuwa bado hajapata ratiba kamili ya wachezaji ambao watasafiri.
''Malengo yetu msimu huu ilikuwa tuchukue ubingwa lakini tumekosa ndiyo maana tunapambana katika mechi zote zilizobakia tushinde kwaajili ya kujiweka katika mazingira mazuri ya kukaa nafasi ya pili'' amesema Bumbuli.
Yanga sc itajitupa dimbani Jumatano ya wiki hii dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Jamhuri huku wakiwa na kumbukumbu ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 nyumbani na Mwadui fc ya shinyanga ilhali Mtibwa wakitoka kupokea kipigo cha bao 1-0 dhidi ya KMC katika uwanja wa nyumbani wa CCM Gairo mjini Morogoro.



