Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yakalia kuti kavu

Jumatano , 23rd Aug , 2017

Mtanange wa Simba na Yanga umekwisha huku Simba SC ikiibuka na ushindi wa Ngao ya Jamii kwa mwaka 2017 huku ikiwalaza watani zao kwa penati 5-4 huku wakiwa wamesawazisha historia ya kila mmoja kuchukua ushindi huo mara 2.

Katika mchezo huo uliobeba hisia za wapenda soka wengi dakika 45 za mwanzo zilimalizika huku timu zote zikiwa hazijaambulia chochote ambapo timu ya Simba SC ikionekana kumiliki mpira kwa asilia 58 huku Yanga wakitawala kwa asilimia 42.

Hata hivyo mpaka inafika dakika ya 90  timu zote mbili yaani siyo Simba wala Yanga aliyeweza kuona lango la mwenzake huku kumbukumbu za mwaka 2010 zikiwa zimejirudia kwenye historia kwa kumaliza dakika zote tisini na kwenda kwenye hatua ya matuta.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na Refa Heri Sasii umekuwa wa hisia sana, kikosi cha Yanga kikiwa kwenye mfumo wa 1-4-3-3 huku Simba wakikimbiza kwa mfumo wa 4-4-2

Akizungumza baada ya mchezo huo Nahodha wa Yanga SC Haroub Cannavaro amewapongeza vijana wake baada ya mchezo huo na kusema kwamba "Vijana wangu wamejitahidi sana japokuwa bahati haikuwa ya kwetu. Nawapongeza kwa kazi kubwa waliyofanya lakini matuta ni mchezo wa kubahatisha na bahati wamepata Simba na ninawapongeza. Tunachotazama sasa mbele ni ligi kuu.

Kwa upande wa penati za Simba zilipigwa na Method Mwanjali, Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima, Shiza Kichuya, Mohamed Hussein huku Penati ya ya nyongeza iliyopigwa na  Mohamed Ibrahim ikiwapa Simba ushindi.

Hata hivyo penati za Yanga zilipigwa na Kelvin Yondani, Tshishimbi, Kamusoko, Ibrahim Ajib, Donald Ngoma,Ngoma pamoja na Husen Tshabalala 

HABARI ZAIDI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi

Wasimamizi wa uchaguzi waongezwe posho - Katambi