Said Ndemla, Hassan Isihaka na Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ ndiyo wachezaji waliokuwa katika kikosi cha Tanzania Bara kilichoshiriki michuano ya Chalenji na kutolewa katika hatua ya robo fainali isipokuwa Waganda wawili, Hamisi Kiiza na Juuko Murshid ambao bado hawajaungana na kikosi hicho.
Ibrahim Ajibu tayari alijiunga na kikosi cha Simba mapema kwa kuwa hakwenda Ethiopia ilipofanyika michuano ya Chalenji baada ya timu kuondoka na kumuacha ambapo awali hakupewa maelezo, lakini baadaye akatakiwa kwenda Ethiopia, lakini hakaueleza uongozi wa TFF hakuwa jijini Dar es Salaam.
