Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Utaratibu ukipoteza cheti cha form 4

Jumatano , 31st Jan , 2018

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia  na Ufundi, William Ole Nasha, amefafanua kuwa Baraza la Mitihani hufanya mchakato wa kutoa vyeti mbadala au uthibitisho kwa mtu aliyepoteza vyeti orijino ndani ya siku 30.

Ole Nasha ameeleza hayo bungeni leo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini, Cosato Chumi (CCM) lililouliza ni utaratibu gani unaotumika pale mtu anapopoteza cheti ili aweze kupata cheti kingine na kama anapata cheti halisi au nakala.

Naibu Waziri huyo amesema kuwa mhitimu aliyepoteza cheti hupatiwa cheti mbadala/uthibitisho wa matokeo baada ya kufuata taratibu kadhaa ikiwemo kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kuhusu upotevu wa cheti na kupata hati ya upotevu. Pia atatakiwa kutangaza gazetini kuhusu upotevu huo.

‘’Mhitimu hutakiwa kujaza fomu ya Baraza la Mitihani baada ya kufuata taratibu zote kisha Baraza hufanya uchunguzi wa uhalali wa umiliki wa cheti husika na kutoa huduma stahiki ndani ya siku 30'', amesema Ole Nasha.

Aidha Ole Nasha amesema kuwa wahitimu waliofanya mtihani kuanzia mwaka 2008 hupatiwa vyeti mbadala huku wale waliofanya mtihani kabla ya Mwaka 2008 hupatiwa uthibitisho wa matokeo ambao hutumwa sehemu unayohitajika.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava