Jumatatu , 28th Jun , 2021

Bodi ya ligi kuu Tanzania TPLB imetoa maelekezo juu ya mashabiki wanaopaswa kukata tiketi, kuzitizama Simba na Yanga katika mchezo wa juni 3 2021 katika uwanja wa Benjamin Mkapa.

Baadhi ya majukwaa ya uwanja wa Taifa

Kwa mujibu  wa taarifa hiyo jumla ya mashabiki 13,782 ndiyo watakaopaswa kukata tiketi mpya  kwa sababu   katika mchezo uliyohairishwa 8  mei  2021 wale waliokata tiketi kwa mfumo wa NCARD  hawatalazimika kulipa tena.

Mgawanyiko wa tiketi 13,782  kama ufuatavyo tiketi  2,218 ni za jukwaa la kijani ( mzunguko) tiketi 11,280 ni  za jukwaa la machungwa  (orange) na tiketi 284  VIP B taarifa imesisitiza  hakutakuwa na tiketi za VIP A  na C zitakazouzwa  kwa ajili mchezo huo wa julai 3

Viingilio  vimepangwa kama ifuatavyo  mzunguko shilingi 7,000, machungwa  10,000 na   kwa upande wa  VIP B kiingilio ni  20,000

Simba na Yanga wanakutana  baada ya  mchezo wao wa tarehe 8 mei kuhairishwa kufuatia sintofahamu iliyozuka baada ya muda wa mchezo kusogezwa mbele, uwanja wa taifa unachukua mashabiki 60,000