Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba yazidi kuisogelea Yanga, mbio za ubingwa VPL

Jumatano , 21st Apr , 2021

Mabingwa wa Tanzania bara klabu ya simba imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliochezwa katika dimba la kaitba huko Bukoba mkoani kagera.

Mshambuliaji wa Simba Luís Miquissone akishangilia baada ya kufunga goli

Mabao ya wekundu wa msimabazi Simba yamefungwa na Luís Miquissone dakika ya 13 na Chris Mugalu dakika ya 24. kwa ushindi huu Simba inafikisha alama 55 ikiwa ni tofauti ya alama mbili na vinara wa ligi Yanga wenye alama 57, wakati Kagera Sugar wanasalia nafasi ya 15 wakiwa na alama 27.

Michezo mingine ya VPL iliyochezwa leo, mchezo wa mapema ulichezwa Saa 8:00 Mchana klabu ya Ruvu Shooting iliibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Mwadui FC  mchezo uliochezwa katika dimba la Mabatini mkoani Pwani, kwa ushindi huo Ruvu wanafikisha alama 37 wakiwa nafasi ya sita kwenye msimamo, na Mwadui wanaendelea kuburuza mkia katika nafasi ya 18 wakisalia na alama 16.

Na klabu ya Mbeya City imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Polisi Tanznaia kweye mchezo uliochezwa mjini Moshi, Kilimanjaro ktika dimba la Ushirika. Bao pekee la mchezo huo limefungwa na Kibu Denis dakika ya 52 na kuipa Mbeya City alama zote tatu, kwa mujibu wa msimamo Mbeya City inafikisha alama 24 wakipanda kwa nafasi moja kutoka ya 17 hadi 16, wakati Polisi wapo nafasi ya 9 na alama 34.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava