Jumatano , 4th Jan , 2017

Mchezaji namba mbili kwa ubora wa tenisi dunia, upande wa wanawake, Serena Williams, amepigwa kipigo cha kushtua na kuondolewa kwenye mechi ya pili ya ASB Classic nchini New Zealand.

Serena Williams

 

Mmarekani huyo mwenye umri wa miaka 35 alifungwa kwa jumla ya seti 4-6 7-6 (7-3) 4-6 na mchezaji anayeshika namba 72, Madison Brengle mjini Auckland.

Mbali ya Serena, pia siku ilikuwa mbaya familia ya Williams baada ya dada yake, Venus, naye kujiondoa kwenye mashindano hayo kutokana na majeraha.