Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Spika Ngudai amtupia kijembe Mwigulu kuhusu Yanga

Jumatatu , 12th Apr , 2021

Kufuatia klabu ya Yanga kutoka sare ya goli 1-1 dhidi ya KMC kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Mkapa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amemtupia kijembe Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mwigulu Nchemba.

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mwigulu Nchemba (kushoto) na Spika wa Bunge Job Ndugai

Spika Ndugai ameanzisha utani huo leo Aprili 12, 2021, bungeni kwenye kikao cha 7, mkutano wa 3 wa bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo amesema wachezaji wa Yanga SC wana njaa hivyo angalau wabunge wawachangie.

"Jana nilimtafuta Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba kwa mambo yetu haya ya bunge akaniambia Spika tafadhali niache, nikauliza sasa nakuacha kuna nini tena? akasema nina 'stress', kumbe matokeo ya juzi yamempa 'stress', pole Mhe. Nchemba na wanayanga wote," - Spika Ndugai

Spika Ndugai akaongeza kwa kusema kuwa, "Taarifa tulizonazo wachezaji wana njaa, maana wamelegea legea hivi, kwa hiyo waheshimiwa wabunge baadaye tunaweza kufanya mchango kidogo tuwasaidie Yanga."

Baada ya sare hiyo, Yanga SC imefikisha pointi 51 baada ya kucheza michezo 24 huku Azam FC wakiwa nafasi pili na pointi 47 ikiwa imecheza michezo 25 na mabingwa watetezi Simba SC wakiwa na pointi 46 wakiwa wamecheza michezo 20.
 

Tazama Video hapo chini
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava