Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Naibu Waziri Mkuu afungiwa maisha

Jumatano , 6th Dec , 2017

Kamati ya Olimpiki duniani IOC imeifungia Urusi kutoshiriki michuano ijayo ya Olimpiki Pyeongchang 2018, sambamba na kumfungia Naibu Waziri Mkuu wa nchi hiyo Vitaly Mutko kutojihusisha na michezo hiyo maisha yake yote.

Vitaly Mutko ni waziri wa zamani wa michezo nchini Urusi aliyehudumu kuanzia mwaka 2008 hadi 2006 alipopata nafasi ya kuwa Naibu Waziri Mkuu.

Mutko amekumbana na rungu hilo baada ya ripoti ya uchunguzi kumkuta na hatia ya kukwamisha zoezi la mamlaka ya kuzuia dawa za kutunisha misuli michezoni (WADA) la kuwachunguza wanamichezo wa Urusi kwenye Olimpiki ya 2014 Sochi.

Bodi ya Utendaji ya IOC pia imewapiga marufuku wanariadha wa Urusi kushiriki michezo ya Olimpiki ya 2018 huko Pyeongchang, Korea ya Kusini lakini imetoa nafasi kwa wanariadha hao kushiriki kama wanamichezo binafsi na sio timu ya taifa.

Mwingine aliyekutana na kifungo cha maisha kutojihusisha na michezo ya Olimpiki ni Yuri Nagornykh, ambaye alikuwa Naibu Waziri wa michezo akimsaidia Mutko wakati makosa hayo ya kukwamisha uchunguzi yakifanyika.

Naye rais wa shirikisho la Olimpiki nchini Urusi (ROC) Alexander Zhukov ameondolewa  uanachama wa IOC, wakati bosi wa zamani wa kamati ya Olimpiki ya Sochi 2014 Dmitry Chernyshenko ameondolewa kwenye kamati ya maandalizi ya Olimpiki ya Beijing 2022.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava