Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mchezaji wa Yanga na Taifa Stars afariki dunia

Ijumaa , 17th Feb , 2017

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Yanga, Prisons na Taifa Stars, Geofrey Bonny 'Ndanje' (37), amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jijini Mbeya alikokuwa akipatiwa matibabu baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya kifua kikuu

Godfrey Bonny 'Ndanje'

Awali taarifa za kuugua kwa kiungo huyo zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, watu wakichangishana pesa kwa ajili ya kumsaidia mchezaji huyo kuendelea kupata matibabu katika hospitali hospitali ya Makandana - Tukuyu wilayani Rungwe mkoani Mbeya.

Dada wa mchezaji huyo aliyepewa nafasi katika timu ya Taifa Stas na kocha Marcio Maximo, Neema amesema, wamempoteza kipenzi chao baada ya kuhangaika naye kumuuguza kwa muda mrefu.

"Tumempoteza ndugu yetu ambaye amefariki usiku wa kuamkia leo, sisi tumekwenda majira ya saa 11:00 alfajiri tukakuta tayari amekwishafariki. Tumekuwa tukimuuguza kwa muda mrefu lakini Mungu amepanga yake, msiba upo nyumbani mjini Mbeya ambako taratibu za mazishi zimekwishaanza," amesema Neema Dada yake Marehemu Bonny.

Bonny alikuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars enzi za kocha Mbrazil, Marcio Maximo na wengi wanamkumbuka kwa soka lake maridadi katika sehemu ya kiungo, licha ya kwamba aliibuliwa wakati umri wake umekwishaenda.

Taifa Stars enzi za Marcio Maximo

Alicheza Yanga chini ya kocha Mserbia, Profesa Dusan Kondic na akaendelea hata alipoondolewa mwalimu huyo na kuletwa Mseribia mwingine, Kostadin Papic.

Ni kati ya wachezaji walioiwezesha Taifa Stars kukata tiketi ya kucheza fainali pekee za michauno ya Ubingwa wa Afrika (CHAN) zinazohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee.  

Hata hivyo, Maximo akamtema katika kikosi cha Stars baada ya fainali za CHAN nchini Ivory Coast mwaka 2009 kutokana na kuwa majeruhi.

Maumivu hayo yalimfanya aachwe na Yanga mwaka 2011 akaenda kumalizia soka yake Simrik SYC ya Nepal.     

 

Bonny akiwa hospitali akipatiwa matibabu hivi karibuni

 

 

 

 

 

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava