Jumatano , 6th Jan , 2016

Baada ya kupoteza pambano nchini Namibia,Bondia Franciss Miyeyusho ameangushia lawama kwa mawakala wanaowapeleka huko kutokutoa tiketi za ndege na malazi kwa wakufunzi ili kuepuka gharama.

Miyeyusho anayecheza uzito waFeatherweight amesema alipoteza pambano hilo kwa kile kinachoaminika upendeleo wa majaji kwa bondia mwenyeji na kukosa maelekezo kwa mkufunzi wake ambaye hajaambatana naye.

Mabondia wengi wa Tanzania wamekuwa wakisaini mikataba ya nje na kuelekea huko bila ya wakufunzi wao,na mwisho wa siku huishiwa kudundwa.

Bondia Nasibu Ramadhani anayecheza uzito wa Bantam naye alikuwa nchini Namibia Novemba mwaka uliopita,kucheza mkatanda wa WBO Afrika uzito mwepesi lakini alipoteza pambano hilo kwa pointi