Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Madeni mawili wanayotakiwa Simba kulipa kwa Yanga

Jumanne , 6th Aug , 2019

Leo ni siku ambayo mashabiki wa Simba wanajigamba kila kona kuwa wataonesha ukubwa wao katika kilele cha tamasha la 'Simba Day' litakalofanyika katika uwanja wa taifa.

Simba na Yanga

Hii ni kufuatia tamasha la watani wao wa jadi Yanga maarufu kama 'Wiki ya Mwananchi' kuhitimishwa, Agosti 4 kwa ufanisi mkubwa pamoja na mchezo dhidi ya Kariobangi Sharks na kutoka sare ya bao 1-1.

Mashabiki wa Simba wakiongozwa na Msemaji wao, Haji Manara wana deni la kulipa kwa Yanga hii leo kwa kuujaza uwanja, kwani waliwacheka Yanga wakisema kuwa licha ya kujaa uwanjani lakini bado kulikuwa na mapengo mengi yaliyoonekana.

Deni la pili kubwa ni la matokeo uwanjani, ambapo katika mchezo wa Yanga na Kariobangi, mashabiki wa Simba walikuwa upande wa Kariobangi na wakionekana kuponda kiwango cha Yanga. Leo hii ni zamu yao wakihitaji kupata ushindi ili kusawazisha mambo.

Simba itacheza na Power Dynamos ya Zambia jioni ya leo. Kuelekea mchezo huo, Haji Manara amesema kuwa mashabiki watarajie mambo mengi ya kushangaza uwanjani, ikiwa ni pamoja na utambulisho wa mchezaji mmoja mpya na wa mwisho.

Pia amejigamba kuwa wao Simba ndiyo waanzilishi wa tukio hilo kwa vilabu hapa nchini kwahiyo wanataka kulifanya kwa namna nyingine. Tusubiri kuona kama Simba wataweza kujibu maswali hayo makubwa mawili hii leo.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava