Katika taarifa yake, Afisa habari wa Coastal Union Oscar Assenga amesema, wameshafanya mazungumzo na timu za Bandari, Small Paka lakini watakapokuwa nchini humo watajua ni timu gani nyingine watakazocheza nazo ambazo zinashiriki Ligi kuu nchini humo.
Assenga amesema, kikosi cha timu ya Coastal kilichopo chini ya Kocha kocha Mganda Jackson Mayanja kinaendelea na mazoezi ya nguvu ili kupambana na changamoto za kiushindani katika michuano ya Ligi kuu.





