
Kocha Jose Mourinho kwenye malalamiko dhidi ya mwamuzi
Wenyeji Real Betis walikuwa wanaongoza kwa mabao 3-2 hadi kufikia dakika ya 57 lakini wachezaji wa Roma walilalamika tukio la mfungaji Alex Moreno aliyeushika mpira kwenye mstari wa goli.
Katika mchezo huo, kiungo Lorenzo Pellegrini alipatiwa kadi ya pili ya njano, wakati kocha Mourinho pia akitolewa nje ya uwanja kwa kupinga maamuzi hayo ya refa.
Gianluca Mancini na Rick Karsdorp nao pia walijikuta wakilambwa kadi za njano za pili katika dakika za mwisho, wakati Betis ikifunga mara mbili na kushinda mabao 5-2.