
Kama ataingia kwenye kikosi cha Liverpool, Isak atakuwa analipwa takriban milioni 780 za Kitanzania kwa wiki, akiwazidi mastaa wengi wa Ulaya kwa kipato. Mshahara huu utamweka nyuma ya Mohamed Salah na Virgil Van Dijk tu, ambao kila mmoja analipwa zaidi ya bilioni 1 kwa wiki.
Wachambuzi wanasema Liverpool wangefanya dili kubwa kwa kumsajili Isak kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kufunga, umri wake mdogo, na uthabiti wake ndani ya EPL. Lakini pia, mshahara wake mkubwa unaashiria matarajio makubwa kutoka kwa kocha na mashabiki.