Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Changamoto za Simba zitanikuzia kipaji

Jumanne , 27th Jun , 2017

Beki wa Kulia wa Klabu ya Simba aliyekuwa akiitumikia Klabu ya Azam FC Shomary Kapombe amewataka mashabiki kuendelea kumpa sapoti katika msimu ujao wa Ligi kuu ya Soka Tanzania Bara.

Kapombe amesema anaamini kutakuwa na ushindani mkubwa ndani ya Klabu ya Simba ambayo alishaitumikia kabla ya kujiunga na Azam FC lakini anaamini changamoto hizo zitamfanya kuwa mchezaji bora zaidi na kuweza kukuza kipaji chake.

“Unajua kufanya maamuzi kama nilivyofanya mimi inatakiwa kuwa na ujasiri, kwani sisi wachezaji tunakuwa na wakati mgumu sana katika kufanya maamuzi kipindi hiki cha usajili, nimetoka Azam FC na kulikuwa na changamoto kubwa ndani na nje ya Klabu, kwa sasa narejea tena Simba na nilianza kuifuatilia tangia msimu uliopita, nilikuwa naiona na naendelea kuiona kwani inawachezaji na benchi la ufundi zuri na naona kunachangamoto kubwa pia ambayo zitanifanya mimi kuendelea kuwa mchezaji mzuri, ” amesema.

“Naamini kiwango changu na ndoto zangu zitaendelea kuwa juu kwani nakutana tena na wachezaji wazuri kama nilipotoka na najua kutakuwa na ushindani mkubwa sana wa namba kwahiyo nimejiandaa na nachukulia changamoto nitakazokutana nazo ndizo zitanipa mafanikio zaidi, ” Kapombe aliongeza.

Shomary amewashukuru uongozi pamoja na mashabiki wa Azam FC kwakuwa naye pamoja na kukiboresha kikosi chake kwa muda wote aliokuwa nao.

“Naushukuru uongozi na mashabiki wa Azam FC kwani najua mchango wao kwangu pia mengi mazuri waliyonitendea, na hapa nilipofikia ni kwa ajili ya Azam FC kwani wamekiwezesha kipaji changu kufikia hapa na naamini nitafika mbali zaidi, ” amesema.

Shomary Kapombe aliitumikia Klabu ya Azam FC kwa miaka mitatu akitokea AS Cannes ambayo alienda akitokea Simba SC na sasa amerudi tena katika Klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava