(Nahodha wa Simba SC, John Rafael Bocco)
Bocco amesema timu yao inapambana kuhakikisha wanarudi kileleni mwa msimamo licha ya ugumu huo ambapo kila kitu kinaenda sawa na malengo hayo yatafikiwa hivi karibuni.
Bocco amesema hayo wakati akizungumzia mchezo wao ujao wa kiporo wa ligi dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa Januari 26 Uwanja wa Kaitaba nakusema kuwa utakuwa mgumu lakini watahakikisha wamapata ushindi .
“Kagera Sugar ni timu bora tunajua mchezo utakuwa mgumu lakini kwa maandalizi waliyofanya wanaamini wataibuka na ushindi licha ya hivi karibuni kutokuwa na matokeo mazuri katika baadhi ya michezo waliocheza. Lakini tutafuata maelekezo tutakayopewa na mwalimu na tunaamini tutafanikiwa,” amesema Bocco.
Kikosi cha Simba kimeondoka asubuhi kuelekea mkoani Kagera tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya wenyeji Kagera Sugar utakaopigwa Jumatano Uwanja wa Kaitaba.