Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ahmed'' Ni furaha kutwaa taji kwa kuifunga Yanga''

Jumatano , 25th Mei , 2022

Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu, Ahmed Ally ameweka wazi kuwa hawana nafasi ya kuchukua taji la Ligi Kuu msimu huu ndiyo maana wameweka nguvu kubwa katika Michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) ambayo Jumamosi watacheza nusu fainali dhidi ya Yanga katika uwanja wa CCM Kirumba

Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu, Ahmed Ally.

Ahmed amesema kuchukua taji la ASFC itakuwa faraja kubwa kwa Wanasimba lakini kuifunga Yanga Jumamosi itakuwa jambo bora litakalotufanya kumaliza msimu kwa furaha.

Ahmed ameongeza kuwa kikosi kinaendelea vizuri na mazoezi na wachezaji waliokuwa wamepata majeraha wanaendelea vizuri na tunategemea watakuwepo kwenye mchezo wa Jumamosi.

“Mlinda mlango Aishi Manula aliumia vidole viwili kabla ya mchezo wetu dhidi ya Geita Gold lakini anaendelea vizuri na anafanya mazoezi ya kucheza mpira na wachezaji wa ndani, na kwa matibabu anayopata tunatarajia atakuwa fiti kabla ya mchezo.

“Shomari Kapombe naye anaendelea vizuri pamoja na Clatous Chama ambaye alianza mazoezi mepesi Jumatatu na wote tunatarajia watakuwa tayari kwa mchezo wa Jumamosi,” amesema Ahmed.

Ahmed amewaomba pia mashabiki wetu kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa CCM Kirumba kwa ajili ya kuisapoti timu kuhakikisha tunaibuka na ushindi.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava