Katibu mkuu wa Chama cha Judo Tanzania JATA Innocent Malya amesema, wamepanga kupeleka wachezaji 14 kati ya 18 walioitwa kwenye kambi ya timu ya Taifa.
Malya amesema, mpaka sasa hakuna mchezaji mwenye uhakika wa kushiriki michuano hiyo kwani makocha watachagua wachezaji wanaostahili kuliwakilisha taifa katika michuano hiyo kutokana na juhudi watakazozionyesha katika mazoezi ya kila siku kambini.
Malya amesema, atakayeonyesha kiwango cha juu ndiye atakayechaguliwa kushiriki michuano hiyo kwani chama kimepanga kutotumika rekodi ya zamani ya mchezaji yeyote.