Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais wa Rotary atoa msaada kwa wanafunzi 800

Jumatatu , 20th Jun , 2022

Rais wa Rotary Kimataifa, Shekhar Mehta leo Juni 20 alitembelea vyombo vya habari vya IPP, ambapo akiwa East Africa TV na East Africa Radio alikabidhi taulo za kike pakiti 10500 zilizotolewa na taasisi yake kwa ajili ya kampeni ya Namthamini.

Rais wa Rotary Kimataifa, Shekhar Mehta (kushoto) akiwa na Mwenyekiti wa IPP, Bw. Abdiel Mengi (kulia) ndani ya ofisi za East Africa TV na East Africa Radio.

Msaada huo wa Rotary utakwenda kusaidia wanafunzi wa kike zaidi ya 800 mashuleni kwa mwaka mzima.

Mwenyekiti wa IPP, Abdiel Mengi amezungumza katika tukio hilo kwa kusema, toka kuanzishwa kwa vyombo vya habari vya IPP waasisi wake walifanya masuala mbalimbali ya kuhudumia jamii, na mpaka sasa kupitia kampeni ya Namthamini imeshawafikia wanafunzi wengi katika mikoa mbalimbali Tanzania.

Rais wa Rotary Oysterbay, Aisha Sykes naye alizungumza kwa niaba ya Rais wa Rotary Kimataifa, kwa kusema tangu waanzishe elimu ya masuala ya hedhi, wameweza kuwajengea uwezo wanafunzi kupitia kampeni ya Namthamini na kuwainua mabinti wanaotoka kaya masikini na kusisitiza wataendelea kuchangia kampeni hiyo.

Pia Rais wa Rotary Kimataifa, Shekhar Mehta siku ya leo alitembelea miradi mbalimbali inayofanywa na taasisi yake katika shule ya sekondari Mtakuja maeneo ya Kunduchi, Dar es Salaam ambayo inagusa hedhi salama na kuinua kiwango cha elimu nchini.

 

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava