Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Huu msiba ni mzito" - Mo Dewji, Mzee Yusuph,GNako

Ijumaa , 24th Jul , 2020

Siku ya Julai 24, 2020 inaingia kwenye kumbukumbu ya Taifa kwa kumpoteza Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa, aliyeiongoza Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 na alizaliwa Novemba 12,1938.

Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Julai 24, 2020

Baadhi ya watu maarufu hapa nchini kuanzia wanasiaisa, wafanyabiashara, na wasanii wameonesha hisia zao kwa kuguswa na msiba huu na kueleza namna gani ambavyo wanamkumbuka Benjamin William Mkapa kupitia mitandao ya kijamii.

"Bado ni ngumu kukubali kwamba Mzee Mkapa hatunaye tena, pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania kwa ujumla kwa msiba huu mzito, Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi, tangulia Baba, nasi tunakuja" ameandika Mfanyabiashara na Mwekezaji wa Klabu ya Simba Mo Dewji.

"Kwake tumetoka na kwake tutarejea, watanzania sote tutakukumbuka upumzike kwa amani Mstaafu Rais wetu" ameandika Msanii Mzee Yusuph

"Tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa kiongozi wetu, mlezi wetu na Rais wetu mstaafu Mh Benjamin William Mkapa, salam za pole ziwafikie ndugu jamaa na marafiki wa marehemu popote pale walipo, tupo pamoja nanyi katika kipindi hiki kigumu na Mungu awatie nguvu" ameandika G Nako Warawara.

"Habari ya kusikitisha sana ambayo nimeamka nayo, Tumempoteza Rais wa awamu ya tatu Tanzania Benjamin William Mkapa, pumzika kwa nguvu ahsante kwa diplomasia yako, mchango wako na huduma zako kwenye jamii" ameandika  Nikki Mbishi.

"Nilipokea habari za Rais Benjamin Mkapa kwa huzuni kubwa, mtu wa kanuni, dhamira thabiti na uadilifu, rehema yangu kwa familia yake, marafiki, wanachama wa Chama cha CCM, na Tanzania nzima kwa ujumla, pumzika kwa amani Mzee Mkapa" ameandika Wakazi.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava