Msanii wa filamu Shamsa Ford
Shamsa Ford amesema anataka kufanya mazoezi na diet kwa wingi ili kupungua kilo 25 ambazo zitamsaidia kwenye afya yake na muonekano wake.
"Nime-miss kaumbo kangu, huu mwaka ni mazoezi sana na diet, nataka kukata kilo 25 na nitaweza kwa ajili ya afya yangu pia kwa ajili ya 'my honey' nisije nikaonekana shangazi yake bure, 2021 muonekano mpya" ameandika Shamsa Ford
Staa mwingine aliyetawala kuhusu muonekano wake ni Wema Sepetu baada ya kupunguza shepu ya mwili wake hadi kufikia kilo 65 kutoka 95.