Jumatatu , 11th Dec , 2023

Komando Lady Jaydee amewataja wasanii Professor Jayt na Mr II Sugu kuwa watabaki kwenye historia ya maisha yake milele kwa sababu wamesimama naye katika kipindi cha kutengwa kwake.

Picha ya Lady Jaydee na Professor Jay

“Ni @ProfessorJayTz na @TheRealJongwe wasanii ambao wamewahi kusimama na mimi katika kipindi cha kutengwa kwangu. Watabaki kwenye historia yangu milele. #ForeverMyBrothers #LadyJayDeeMemoir” - ameandika Lady Jaydee kupitia page yake ya X.

Tayari Lady Jaydee ameshafanya ngoma kadhaa na wakongwe hao wa muziki Tanzania zikiwemo Sugu ft Lady Jadydee ‘Muda mrefu’ na ‘Mambo ya Fedha’ pia nyimbo alizofanya na Prof Jay ni Bongo Dar es Salaam, Nimeamini na Joto Hasira.