Ijumaa , 24th Jun , 2016

Mtayarishaji wa muziki wa kizazi kipya Lufa amefunguka ndani ya Enews kuhusiana na doto zake za kufanya kazi na Rapa mahiri duniani Wiz Kid, huku akisema atafurahi sana siku atakapo pata nafasi na kufanya kazi na rapa huyo machachari.

WIZ KID

Lufa amesema studio ya Swich Record ambayo inamilikiwa na msanii QUICK ROCKA ndiyo studio yake ya kwanza kufanya kazi na tayari amekwishatoa ngoma kali kibao ikiwemo watabamba na nyingine kibao ambazo zilishika chati kwenye stesheni za radio mbalimbali.

Hata hivyo Lufa kasema ana uwezo wa kutengeneza hadi biti tano kwa siku kwahiyo anakaribisha wasanii wa aina zote za muziki na gharama zake ni laki tano kwa wimbo mmoja na ndoto zake ni kufanya ngoma nyingi zaidi bila kuchagua ili kuweza kujitangaza kimataifa.