Jumanne , 8th Dec , 2020

Kufuatia kuzungumziwa kwenye kurasa za kidaku kwenye mtandao wa Instagram kwamba anashea wapenzi wawili kwa wakati mmoja, mtangazaji King Smash amefunguka kusema hawezi kufurahia kwa kilichotokea bali ni masuala ya kipuuzi.

Mtangazaji wa East Africa TV King Smash

Taarifa hiyo iliripoti  kuwa mtangazaji huyo anashea mahusiano na wanawake wawili tofauti na  wanafanya kazi pamoja ambao ni Tina ripota wa show ya eNewz ya East Africa TV na Dolly Dolly mtangazaji wa The Base ya ITV.

King Smash amesema watu wanafuta 'content' za kuzungumziwa ili kujiingizia pesa kupitia yeye ila binafsi anaona suala hilo haliwezi kumshusha wala kumpandisha kwenye upande wake wa kazi.

"Sina 'comment' yoyote kuhusiana na hilo, mimi huwa sizungumzii ujinga pia siwezi kutolea ufafanuzi vitu vya kipuuzi na udaku, siwezi kukwazika wala kufurahi kwa kilichotokea kwani watu wanaingiza pesa kupitia mitandao ya kijamii wanatafuta 'content' kwa kuwazungumzia watu fulani ili wao wapate pesa hizo" amesema King Smash 

Tumejaribu kuwatafuta wanawake wote wawili ili kuweza kufanunua suala hili kwa bahati mbaya hawakuweza kuonyesha ushirikiano wowote.