Jumatatu , 3rd Nov , 2014

Mrembo aliyenyakua taji la Miss Kenya kwa mwaka 2014, Idah Nguma ameweka wazi mpango wake wa kuanzisha taasisi ya Hisani kwa ajili ya kuongeza nguvu katika mapambano ya ugonjwa wa saratani ya kizazi na matiti, hususan kwa wanawake.

Miss Kenya 2014 Idah Nguma

Idah amesema kuwa, mpango huu umemjia kutokana na yeye binafsi kumpoteza rafiki yake wa karibu kwa ugonjwa huu hatari wa saratani.

Idah ambaye ni Msomi wa masuala ya Masoko kutoka katika Chuo Kikuu cha Kenyatta, kwa sasa pia anajiandaa kwa ajili ya kuiwakilisha nchi yake katika mashindano ya urembo ya Miss World mwezi Desemba mwaka huu.