
Marehemu Maalim Muhidin Gurumo
Kwa mujibu wa mtoto wa kwanza wa Marehemu, Abdallah Gurumo kwa sasa msiba bado upo Mabibo ambapo jioni ya leo kutafanyika kisomo maalum kwa minajili ya taratibu za dini ya Kiislamu kwa ajili ya marehemu.
Marehemu Gurumo alifariki dunia jana jioni katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na maradhi ya moyo ambayo yamekuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.
Unaweza kumsikiliza msemaji wa Familia ya Gurumo, Bwana Yahaya Mikole akieleza ratiba nzima ya msiba hapa;