Ijumaa , 15th Jun , 2018

Msanii  wa Bongo fleva Bill Nass, amesema kuwa  anatamani kuajiriwa ili afanyie kazi  'course' aliyosomea chuo katika shahada yake.

Akizungumza na www.eatv.tv Bill Nass amesema  endapo atapata kampuni itakayo mtambua yeye kama msanii na kumpa uhuru kuendelea  kufanya mziki,basi  yupo tayari kufanya kazi.

"Sitaki kuingia kwenye kampuni ya mtu nibanwe na unajua mtu yeyote anaanzisha kampuni kupata faida, kwahiyo nataka ile kazi ambayo nitafanya kila mtu apate chake na niwe free na kufanya mziki wangu na kama show itatokea kusafiri basi iwe tayari kunielewa". Amesema Bill Nass

Bill Nass amemaliza kwa kusema kuwa anaogopa kufanya kazi kwakuwa mziki una vitu vingi kama kusafiri kwahiyo hataki kubanwa na kazi na kumpelekea kuacha mziki ila endapo akipata kampuni ambayo iko tayari kuelewa anachokifanya,  basi hana budi kufanya nao kazi.