
Jude Bellingham
Muingereza huyo mwenye umri wa miaka 22 alipata jeraha hilo Novemba 2023 katika msimu wake wa kwanza ndani ya Real Madrid katika mchezo dhidi ya Rayo Vallecano lakini alikuwa akighairisha zoezi hilo ili aisaidie klabu yake na huku akitumia dawa za kumpa nafuu kwa muda.
Licha ya kupambana kuisaidia Los Blancos imalize na mataji msimu huu, jitihda zake zimegonga mwamba baada ya kumaliza msimu wa 2024-2025 bila taji lolote baada ya hapo jana kupoteza nusu fainali ya klabu bingwa ya Dunia 4-0 dhidi ya PSG.