Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zumaridi hana kesi ya kujibu - Mahakama

Jumanne , 6th Dec , 2022

Kesi namba 12 ya mwaka 2022  inayomkabili Diana Bundala maarufu kama Zumaridi na wafuasi wake 84 ya kufanya mkusanyiko usio halali leo hii mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Mwanza imesema Zumaridi na wafuasi wake 80 hawana kesi ya kujibu huku wafuasi watatu wakikutwa na kesi ya kujibu

Akisoma maamuzi hayo Hakimu mkazi Clescensia Mushi amesema mahakama imejiridhisha pasina shaka kuwa washtakiwa walioachiwa hawakuguswa na vipengele muhimu vinavyotakiwa katika kuthibitisha makosa ya jinai kwa mujibu wa sheria.

Hakimu Clescensia amewataja washitakiwa watatu waliopatikana na kesi ya kujibu kuwa ni Juma Hamisi ambae ni mshitakiwa namba 5, Meshak Joseph mshtakiwa namba 33 na Daud Manyanda mshtakiwa namba 45

Amesema washitakiwa hao ndio pekee waliotajwa na mashahidi wa Jamhuri kuwa ndio waliosababisha majeraha na maumivu makali dhidi ya askari waliokwenda nyumbani kwa mfalme Zumaridi kuwakamata Februari 23 mwaka huu.

Amesema maamuzi hayo ya kuwaachia washtakiwa 81 yametokana na upande wa Jamhuri kushindwa kujenga kesi yao yaani "Premafacie" kwani mashahidi wake  walishindwa kutambua washitakiwa kuwa walitenda makosa au la.
Baada ya maamuzi hayo hakimu Mushi akaiahirisha kesi hiyo hadi Decemba 20, mwaka huu itakapokuja kwa kwa ajili ya utetezi kwa washitakiwa watatu waliopatikana na kesi ya kujibu.

Katika hatua nyingine kesi namba 10/2022 ya kuwazuia maafisa wa serikali kutekeleza majukumu yao inayomkabili Zumaridi na wenzake nane imeendelea leo huku upande wa Utetezi ukileta mashahidi wawili kwa lengo la kutoa utetezi wao.

Mashahidi hao wametoa utetezi wao leo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Monica Ndyekobora na kuiambia mahakama kuwa waliwaona Askari polisi nyumbani kwa Zumaridi wakivunja mageti na kupiga mabomu ya machozi na kufikishwa polisi na baadae mahakamani.

Baada ya kusikiliza ushahidi huo Hakimu Ndyekora akaiahirisha kesi hiyo hadi kesho Desemba 7 mwaka huu atakapoendelea kusikiliza ushahidi kwa mashahidi wawili waliobaki.

HABARI ZAIDI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi

Wasimamizi wa uchaguzi waongezwe posho - Katambi