Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waziri Mkenda aweka wazi mchakato wa Mitaala mipya

Jumatano , 18th Mei , 2022

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda amesema Serikali ina mpango kabambe wa kukimbiza na kuyafanyia haraka mageuzi ya elimu ambapo kufikia mwezi Disemba 2022 rasimu ya Mitaala mipya pamoja na rasimu ya mapitio ya sera itakuwa imekamilika.

Prof Adolf Mkenda ameyasema hayo leo tarehe 18 Mei 2022 Ofisini kwake Jijini Dodoma wakati alipokutana na kuzungumza na Mwakilishi Mkazi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa Bw Zlatan Milisic.

Waziri Mkenda amemuhakikishia mgeni wake kuwa serikali ya Tanzania imejipanga vyema na kufikia Mwezi Januari mwaka 2023 inatarajia kuanza mchakato wa kufanya maamuzi baada ya Rasimu hiyo kuwa imekamilika.

Waziri Mkenda ameeleza kuwa Umoja wa Taifa umeandaa mkutano maalumu unaotarajiwa kufanyika mwezi Septemba mwaka huu Mjini New York nchini Marekani kujadili mageuzi makubwa ya elimu Duniani.

Waziri Mkenda ameeleza kuwa Mkutano wa wakuu wa nchi utaanzisha mchakato katika nchi nyingi Duniani lakini wakati zinaanza mageuzi hayo ya elimu tayari Tanzania itakuwa imefikia hatua nzuri za maamuzi hivyo kwenda mbele kwa haraka Zaidi.

Prof Mkenda amesema kuwa mchakato huo wa magezi hayo nchini Tanzania umetokana na maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan aliyotoa wakati akilihutubia Bunge la Tanzania tarehe 22 Aprili 2021 kuhusu mabadiliko ya Mitaala ya elimu na muelekeo mpya katika sekta ya elimu aitakayo.

“Na mimi niwahakikishie tu kuwa Kupitia umoja wa Mataifa ni rahisi kujua nchi zingine zinafanya nini kwenye sekta ya elimu ili kuweza kuboresha sekta yetu” Amekaririwa Prof Mkenda na kuongeza kuwa

Amemuahidi Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Prof Adolf Mkenda kuendeleza ushirikiano ili kuhakikisha kuwa malengo ya maboresho kwenye elimu yanatimia ili elimu itolewayo iendelee kuwa bora.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava