Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu wanne kizimbani kwa uhujumu uchumi

Jumatano , 16th Sep , 2020

Watu wanne wamefikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kkisutu Jijini Dar es Salaam wakikabiliwa na mashitaka ya uhujumu uchumi, ikiwemo kujihusisha na usafirishaji wa dawa za kulevya aina ya heroin kilo 51.47.

Washitakiwa hao ni Ernest Michael Semayoga, Salum Jongo, Amini Sekibo na Tatu Nassoro ambao wamesomewa mashitaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Cassian Matembele na mawakili wa serikali Paul Kadushi, Wankyo Simon na Benson Mwaitenda.

Imedaiwa Mahakamani hapo kwamba kati ya mwezi Septemba mwakam 2020 katika Mtaa wa Veterinary Temeke mkoa wa Dar es Salaam walijihusisha na kuwa na dawa za kulevya aina ya heroin kilo 51.47.

Katika shitaka la pili washitakiwa wote kwa pamoja kati ya Septemba 1 na 8 mwaka 2020 katika Jiji la wa Dar es Salaam walitenda kosa la utakatishaji fedha haramu kwa kujipatia kwa njia ya udanganyifu fedha za kitanzania shilingi milioni 62,370,000, fedha za Msumbiji 7,370, Fedha ya Kenya shilingi 400, na magari manane ya aina tofauti.

Katika shitaka la tatu ndani na nje ya mkoa wa Dar es Salaam kati ya Septemba 1 na 8 mwaka 2020 inadaiwa washitakiwa walitenda kosa la kuongoza genge la uhalifu kwa kusafirisha dawa za kulevya aia ya heroine kilo 51.47.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 30 na washitakiwa wataendelea kusota rumande kutokana na makosa hayo kuwa hayana dhamana.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava