Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wasomi tukumbuke kuisaidia jamii yetu - Rebeca

Jumanne , 27th Sep , 2016

Mwanaharakati wa kupinga ndoa za utotoni nchini Tanzania Rebeca Gyumi amewataka vijana ambao wamepata nafasi ya kusoma na kupata elimu, kukumbuka kuisaidia jamii katika mambo yanayowakwamisha kimaisha.

Mwanaharakati Rebeca Gyumi akionesha tuzo aliyopewa na UNICEF akiwa katika studio za EA Radio

Rebeca ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali, Msichana Initiative linalotetea haki za wasichana kupata elimu, ameshinda tuzo ya Umoja wa Mataifa inayotolewa kupitia UNICEF katika kipengele cha mabadiliko ya kijamii.

Ametoa ujumbe huo alipokuwa katika kipindi cha SUPAMIX alipokuwa akielezea namna ambavyo ameweza kutambulika na kupewa tuzo na shirika la UNICEF kupitia Umoja wa Mataifa.

“Hakuna kitu kizuri kwangu kama kutumia elimu yangu kusaidia jamii ambayo nimeilelewa, mimi ni zao la jamii kuona kwamba elimu niliyopata kuna watu walijinyima ili mimi niweze kusoma, ndiyo maana natumia nilichokipata kuweza kurudisha angalau fadhila za jamii yangu” Amesema Gyumi.

Rebecca ameongeza kuwa ni vyema viongozi ndani ya jamii yetu wakiwafundisha vijana namna ya kuitumikia jamiii yetu kuliko vijana wa kitanzania kufundishwa na mataifa mengine juu ya namna ya kuwa kiongozi bora ndani ya jamiii kwa kuwa jamii ya kitanzania itaendelezwa na watanzania wenyewe .

Kutokana na ujasiri aliouonesha wa kufungua kesi dhidi ya serikali kuhusu sheria ya ndoa iliyokuwa inatoa fursa kwa mabinti wadogo kuolewa ndipo UNICEF ikaweza kumtunuku tuzo ya kutambua mchango wake, shughuli ambayo ilifanyika nchini Marekani.

HABARI ZAIDI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi

Wasimamizi wa uchaguzi waongezwe posho - Katambi