
Lori la basi yaliyogongana Morogoro
Ajali hiyo imetokea leo Julai 20, 2022, majira ya saa 3:00 asuhubi, ambapo baadhi ya abiria waliokuwa kwenye basi hilo wamesema kuwa kilichosababisha ni kutozingatiwa kwa sheria za barabarani wakiomba jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kuongeza umakini ili kupunguza ajali zisizo za lazima.
Mkuu wa Upelelezi mkoa wa Morogoro ACP Ralph Meela, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo chanzo cha ajali kinadaiwa kuwa ni uzembe wa dereva wa basi hilo Hassan Abdallah ambaye alikuwa akijaribu kulipita gari lingine bila kuchukua tahadjari na kusababisha ajali hiyo.