
Paul Pogba
Paul Pogba mwenye umri wa miaka 32 amewahi kucheza kwa mafanikio makubwa akiwa na Juventus ya Italia akiisaidia Kibibi Kizee cha Turin kuchukua kombe la Serie A mara nne, Super cup mara tatu pamoja na Coppa Italia mara tatu.
Kiungo huyo aliyeshinda kombe la Dunia 2018 akiwa na timu yake ya taifa ya Ufaransa anatarajiwa kurejea katika ardhi yake ya nyumbani baada ya kuanza mazoezi wiki kadhaa zilizopita kabla ya kuanza kipindi cha pre season
Pogba alikuwa nje ya uwanja kwa msimu mzima baada ya kufungiwa kutokana na kukutwa na hatia ya kutumia dawa zilizozuiliwa michezoni .