Jumanne , 16th Jul , 2024

Bodi ya ligi kuu Tanzania Bara (TPL) imetangaza rasmi msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2024-25 unataraji kuanza mnamo Agosti 16-2024 huku michezo ya ufunguzi ya ligi hiyo maarufu kama michezo ya ngao ya jamii yaani Community Shield inataraji kuanza kuchezwa kati ya Agosti 8 mpaka 11-2

Taarifa ya TPLB imeeleza kuwa ligi hiyo inataraji kumalizika mnamo Mei 24-2025  huku ikihusisha mizunguko 30 huku dirisha dogo la Usajili likitaraji kufunguliwa Desemba 15 mpaka Januari 15-2025

Bingwa Mtetezi wa ligi kuu Tanzania Bara msimu uliopita 2023-24 ni klabu ya Yanga SC huku timu mbili ambazo zimepanda kwa msimu huu ni pamoja na timu za Kengold FC kutoka Tukuyu Mbeya na Pamba Jiji FC kutoka Mwanza

Upande mwingine,Ligi daraja la Kwanza maarufu kama Championship yenyewe inataraji kuanza mnamo Septemba 14-2024 huku ikitaraji kumalizika mnamo Mei 10-2025 huku mchezo wa fainali ya kombe la FA utachezwa mnamo Mei 31-2025