Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanahabari watakiwa kupata elimu ya ukatili

Jumanne , 17th Mei , 2022

Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria, Bi. Mary Makondo amewataka wahariri  na waandishi wa habari kupata mafunzo maalumu kuhusu kuripoti taarifa zinazohusiana na vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii zetu.

Amesema hayo wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili ya namna ya utoaji taarifa za ukatili wa kijinsia kwa Wahariri na Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini , mafunzo yaliyofanyika jijini Arusha.

Bi. Makondo amesema lengo la mafunzo hayo ni kujengeana uwezo, kujifunza, kubadilishana uzoefu, mbinu na kujadiliana kuhusu nafasi ya Waandishi wa Habari na Wahariri katika kutokomeza ukatili wa kijinsia katika jamii zetu.

Bi. Makondo amesema kumekuwa na ongezeko la matukio ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na uhalifu kama vile, ubakaji, ndoa za utotoni, ukeketaji, ukatili wa majumbani, wajane kupokwa mali za wenza wao na mauaji. 

"Katika kukabiliana na ukatili wa kijinsia, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wadau wake katika mapambano hayo. Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kuimarisha mifumo ya kisheria na utoaji haki, huduma za afya, elimu, kuanzisha vituo vya huduma kwa manusura wa ukatili na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola, ikiwemo mahakamani wote wanaotuhumiwa na makosa ya ukatili. " amesema Bi. Makondo. 

Aidha, Serikali imewezesha kutungwa kwa sheria ya Msaada wa kisheria kwa lengo la kumeimarisha upatikanaji haki kwa watu wasio na uwezo wa kumudu gharama za mawakili. Kwa sasa Wananchi wana uwezo wa kutafuta na kupata afua za kisheria kwa kutumia njia mbadala za utatuzi wa migogoro nje ya Mahakama. Haya yote ni juhudi za Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria na kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Wahariri na Waandishi wa habari.

Bi. Makondo ametoa rai kwa Wanahabari kuzingatia maadili ya uandishi na kulinda waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia wakati wa utoaji taarifa ili kuepuka athari zaidi kwa wahanga wa matukio haya.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava