
William Ole Nasha
Mhe. Ole Nasha ameyasema hayo kwenye mahojiano maalum na EATV ilipotaka kujua serikali imefanya jitihada gani katika kuweka mazingira wezeshi kwa wafugaji ili waweze kufuga na kuzalisha kwa tija.
Amesema katika kuhakikisha mifugo inachangia katika kukuza pato la taifa na mtu mmoja mmoja serikali tayari imeanza kuwafundisha wafugaji kufuga kibiashara na kuwaboreshea miundombinu bora.
Kwa upande wa ujenzi wa viwanda vya nyama amesema tayari wameanza ujenzi wa kujenga viwanda vya kuchakata nyama nchini.