Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

VIDEO: Mrema awahurumia wafungwa

Ijumaa , 19th Mei , 2017

Mwenyekiti wa bodi ya Parole Taifa, Mh. Augustino Lytonga Mrema amefafanua na kusema sababu kubwa ya msongamano wa wafungwa Magerezani ni pamoja na wanachi kupenda kesi na visasi kwa kushindwa kumalizana mitaani, hivyo kuwataka kutoendekeza visasi .

Leo akifunguka kwenye East Africa Breakfast ya EA radio Mh. Mrema amesema kuwa wananchi wamekuwa sababu ya misongamano magerezani kwani kesi nyingine ni ndogo  za kuweza kumalizana nyumbani lakini wanaamua kukomoana kwa kupelekana polisi hadi kufikia kufungana.

Aidha Mh. Mrema ameongeza kwamba kuna wafungwa waliopo Magereza kwa kukosa watu wa kuwalipia faini hivyo ametoa nafasi kwa watu watakaoweza kufanikisha zoezi hilo waweze kuwasaidia  ndugu zao ikiwa ni pamoja na kuwaepusha na maradhi yapatikanayo kwenye msongamano wa magereza

"Kama Mume wako au mtoto wako amefungwa kwa kukosa faini unaruhusiwa kumlipia. ni vyema mkatumia nafasi ya sheria hii ili kuepusha msongamano magerezani. Lakini mnatakiwa kutambua kwamba kule siyo kuzuri na watu wanajifunza tabia mbaya na magonjwa mengi yanapatika kule, wasaidieni. Jukumu la kupunguza msongamano ni la wana ndugu"- alisema Mrema.

Pamoja na hayo Mh. Mrema ameongeza kuwa tayari ameshaliomba jeshi la polisi kuacha kuhangaika na mateja wasiojiweza kuwapeleka magereza bali wasaidiwe kwa kupelekwa vituo vya kuwasaidia waathirika wa dawa lakini pia wahakikishe wanaowapeleka magereza wawe mapapa wa dawa za kulevya ambao ni chanzo cha mateja nchini.

Mtazame Mh. Mrema hapa chini akifunguka kwa undani zaidi.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahundi - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava