
Kushoto ni Balozi wa Ujerumani nchini Regina Hess na kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Emmanuel Tutuba
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Emmanuel Tutuba, amesaini mkataba wa ushirikiano na serikali ya Ujerumani ambapo bilioni 14.2 ni kwa ajili ya mradi wa kukabiliana na mwingiliano wa wanyamapori na binadamu, na bilioni 7.1 ni za kusaidia upatikanaji wa haki kwa wanawake na watoto, huku bilioni 2.4 zikielekezwa katika utafiti na maandiko.
"Baada ya kuhifadhi wanayama wetu tunaona wameongezeka na kuvamia wananchi na mashamba ya jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi zetu, sasa sekta ya utalii katika mradi huu imeepewa zaidi ya bilioni 6 ambazo zitaenda kusaidia kukabiliana na athari za mwingiliano wa wanyamapori na binadamu," amesema Dkt Tutuba
Akizungumza kwa niaba ya serikali ya shirikisho la Ujerumani, Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania amesema kwamba baada ya kushirikiana katika miradi ya maji na afya, sasa wanakwenda kusaidia jamii zinazozunguka hifadhi huku viongozi wa Wizara ya maliasili na Utalii pamoja na Katiba na Sheria wakiahidi kusimamia matumizi sahihi ya fedha hizo.